Fikra

Mpango wa mafunzo ya mbali kwa Muislamu mpya anayezungumza Kiswahili, unaolenga kumfundisha majukumu muhimu ya dini, jinsi ya kuishi kwa mujibu wa Uislamu, na jinsi dini hii inavyoleta athari chanya katika maisha yake, roho yake, furaha yake, na elimu yake. Lengo ni kumwezesha kumwabudu Mwenyezi Mungu kwa elimu na upeo sahihi, na kumwandaa kuwa mlinganizi wa dini ya Mwenyezi Mungu.


    Malengo ya Programu

  • 1.Kuimarisha uelewa wa msingi wa Uislamu: Kutoa elimu ya msingi kuhusu itikadi na ibada za Kiislamu kwa Waislamu wapya.
  • 2.Kusaidia ujumuisho wa kiroho na kijamii: Kuwasaidia Waislamu wapya kujiunga na jamii ya Kiislamu na kukuza hisia ya kuwa sehemu ya umma wa Kiislamu.
  • 3.Kuwafundisha misingi na kanuni za dini: Kuwawezesha Waislamu wapya kutekeleza ibada zao kwa kujiamini na kwa maarifa sahihi kulingana na Qur’an na Sunna.
  • 4.Kufundisha maadili ya Kiislamu: Kuweka misingi ya maadili na tabia njema za Kiislamu zinazoimarisha mwenendo mzuri na uhusiano mwema na wengine.
  • 5.Kutoa msaada wa kudumu: Kuunda mtandao wa msaada endelevu kwa Waislamu wapya, unaotoa ushauri na mwongozo katika nyanja zote za maisha yao.
  • 6.Kukuza ujuzi wa da'wa: Kuwanoa washiriki ili wawe walinganizi wenye ushawishi katika jamii zao, wenye uwezo wa kueneza ujumbe wa Uislamu kwa ufanisi na kuendeleza uongozi wa Kiislamu kwa ajili ya maendeleo ya jamii.
  • 7.Kuhimiza elimu endelevu: Kuwahamasisha washiriki kuendelea na kujifunza dini yao na kuongeza maarifa yao ya Kiislamu kwa muda mrefu.




Ubora

Matokeo ya Diploma


Baada ya kukamilisha diploma, mhitimu atakuwa na uwezo wa:

* Kuelewa na kutekeleza nguzo za Imani na Uislamu kwa usahihi.
* Kutekeleza ibada za msingi kwa mujibu wa Sunna ya Mtume ﷺ.
* Kutumia sheria za Kiislamu (fiqhi) katika maisha yake ya kila siku.
* Kujipamba na maadili ya Kiislamu katika maisha yake binafsi na ya kijamii.
* Kushiriki kwa ufanisi katika jamii ya Kiislamu na kueneza Uislamu kwa wasio Waislamu.

Kwa atayemaliza atapata:

1- Cheti cha kumaliza programu.
2- Usajili bure katika diploma ya Akademia ya Kiislamu ya Afrika.
3- Cheti cha kujiunga na moja ya vituo vya Kiislamu.
4- Zawadi kumi za fedha kwa wanafunzi kumi bora.

Motisha kwa wanafunzi wanaoshiriki:

* Vyeti vinavyotambulika: kila mwanafunzi atapata cheti kinachotambulika kutoka kwa akademia.

Zawadi za kuhamasisha:


Msaada wa kifedha kwa wanafunzi bora mwishoni mwa diploma.
• Vitabu na rejea mbalimbali bure: Kutoa vifaa vya kujifunza vya kielektroniki bure kwa washiriki.
* Safari za kielimu: Kuandaa ziara katika misikiti na taasisi za Kiislamu ili kuimarisha kujifunza.


Majina ya washindi

🏆 Majina ya Washindi wa Shindano la Walimu

🎉 Hongera sana! Mungu akubali kutoka kwako, akulipe, na akuinue hadhi yako 🌷

📍 Ili kuwasiliana na Akademia kuhusu Zawadi na kupokea what’s up

Zawadi za kifedha:


Walimu watano bora zaidi watapata tuzo za kifedha:


  • 🥇 Wakwanza: 200,000 za Kitanzania
  • 🥈 Wapili: 180,000 za Kitanzania
  • 🥉 Watatu: 150,000 za Kitanzania
  • 🏅 Wanne: 120,000 za Kitanzania
  • 🏅 Watano: 100,000 za Kitanzania
Nchi Jina la Mshindi Zawadi Daraja Nafasi
Tanzania RASHID MOHAMED HAMISI 200,000 za Kitanzania 100% Wakwanza
Kenya سالم براسا 180,000 za Kitanzania 100% Wapili
Kenya أوكتي آدم سكوى 150,000 za Kitanzania 100% Watatu
Kenya Muhammed Maero Namati 120,000 za Kitanzania 100% Wanne
Kenya ISRAI ABDALLAH JUMA 100,000 za Kitanzania 100% Watano